Skip to main content

Simulizi : Kifo Siku Ya Harusi Yangu Sehemu Ya Kwanza (1)

Simulizi : Kifo Siku Ya Harusi Yangu

Sehemu Ya Kwanza (1)

IMEANDIKWA NA : ERIC SHIGONGO

********************************************************************************

Simulizi : Kifo Siku Ya Harusi Yangu

Sehemu Ya Kwanza (1)

MWANZO

Mamia ya watu walikuwa wamefurika ndani ya ukumbi wa Pundamilia ulio ndani

ya hoteli ya maarufu ya Atrium, karibu kila mtu maarufu nchini Tanzania alikuwa

ndani ya ukumbi huu. Kuanzia Rais, Mawaziri, Makatibu Wakuu, wanamichezo,

wasanii na wafanyabiashara wakubwa wa Kiasia na Afrika. Hakika ilionekana siku

ya furaha, watu wakiwa wameketi kwenye meza zao wakiendelea kunywa

vinywaji taratibu.

Wanaume wakiwa wamevalia suti nyeusi na wanawake magauni ya rangi nyeupe

na zambarau, hakika walipendeza. Kila nilipozungusha macho yangu huku na kule

ndani ya ukumbi nilionekana kutoamini kilichokuwa kinatendeka, hatimaye 

baada ya safari ndefu ya kupanda na kushuka milima, nilikuwa namuoa Bianca

Rwegoshora, mtoto wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano

wa Tanzania.

Wazazi na ndugu wa pande zote mbili walionekana kufurahia kila kitu kilichokuwa

kikitokea ukumbini, kwao hakika ulikuwa ushindi, walikuwa wamefanikisha

kutokea kwa jambo ambalo kwa muda mrefu walilihangaikia sana, kuhakikisha

kwamba namuoa Bianca badala ya Farida Mbaraka, kisa tu alikuwa ni mtoto

aliyetokea familia duni, wazazi wake wakiwa hawana elimu hata ya darasa la saba.

Hicho ndicho kilikuwa kikwazo, hakuna aliyeuangalia uzuri wake, wala ukarimu

wa moyo wake, alihukumiwa sababu ya umasikini wake, hakika iliuma.

Asilimia kubwa ya ndugu zangu waliokuwa ukumbini, macho yangu

yalivyowapitia, sikumpata hata mmoja ambaye hakuwa na digrii! Wengi walikuwa

ni madaktari, maprofesa, wenye elimu ya chini kabisa walikuwa ni wenye digrii

moja pamoja na wanafunzi waliokuwa vyuoni na sekondari ambao pia

walitegemea kuingia kaburini wakiwa na digrii si chini ya tatu.

Hiyo ndiyo ilikuwa familia yangu, familia ya wasomi, walioheshimu watu kwa

alama zilizotangulia majina yao, mfano Dk., Injinia, Mchumi, Mwanasheria, n.k.

Mtu yeyote ambaye hakuwa na vitangulizi vya taaluma yake, hakuheshimiwa na 

familia yangu. Hicho ndicho kilichompata Farida Mbaraka, kwa sababu ya familia

yake kutokuwa na elimu, alionekana kama kinyaa, ingawa nilimpenda mno, baadhi

ya ndugu zangu waliomo ukumbini wakishangilia, walimkashfu na kusema

kwamba kumuoa ingekuwa ni kutumia sheria iitwayo “The Dilution Law”.

“Mtoto huchukua akili kutoka kwa baba na mama, ukiwa na akili nyingi, halafu

ukaoa mwanamke au kuolewa na mwanaume asiyekuwa na akili, mtoto wako

atakuwa na akili kidogo, lakini ukioa mwanamke au kuolewa na mwanaume

mwenye akili nyingi, lazima watoto wako watakuwa vipanga sana darasani!” Hayo

yalikuwa ni maneno ya Joackim, mtoto wa baba yangu mkubwa ambaye yeye

katika umri wa miaka thelathini tu alikuwa anasomea digrii ya tatu nchini

Marekani. Alikuwepo ukumbini akishangilia juhudi zake za kuhakikisha simuoi

Farida bali Bianca, ambaye karibu familia yake yote ilikuwa ni ya wanasheria.

“Genesis!” Ilikuwa ni sauti ya Bianca akiniita, nikageuza kichwa changu

kumwangalia, ili kumfanya asigundue kwamba nilikuwa na mawazo, niliusogeza

mdomo wangu karibu na wake na kumbusu, wapiga picha wakafanya kazi yao.

“Yes sweetie!” (Ndio mpenzi)

“What is going on your mind?”( Nini kinaendelea kichwani mwako?)

“Why?”(Kwanini?)

“You seem to be contemplating too hard!”(Unaonekana kufikiria sana)

“No! I am just thinking about our future, where we have come from, where we are

and where we are going!”(Hapana! Nafikiria tu kuhusu maisha yetu ya baadaye,

tulikotoka, tulipo na tunakokwenda!)

“Isn’t Farida on your mind?”(Farida hayupo kichwani mwako?)

“Me? No way! That drug dealer? Probably she is dead by now.”(Mimi? Huyo muuza

madawa ya kulevya? Labda amekwishakufa tayari) niliongea nikichukua kitambaa

na kujifuta machoni.

Si kweli kwamba nilikuwa simpendi Farida, kila jina lake lilipotajwa huzuni

iliniingia na machozi kunilengalenga, nilimpenda sana msichana huyo na katika

maisha yangu sikuwahi hata mara moja kukutana na msichana wa aina yake.

Alikuwa na sifa zote, kuanzia uzuri wa sura na maumbile mpaka tabia na

mwenendo wake na hicho ndicho nilichohitaji kutoka kwa mwanamke wa kuishi

naye maisha, sifa ambazo wazazi na ndugu zangu katu hawakuziona, kwao kitu

cha muhimu kilikuwa ni elimu.

“Then why are you so sad? Are you not happy that we are finally married?”(Sasa

kwanini una huzuni siku ya harusi yetu? Haufurahii kwamba hatimaye

tumeoana?)

“I am so happy and excited, though I can’t stop myself thinking of Farida.”(Nina

furaha sana ingawa siwezi kujizuia kumfikiria Farida)

“But a few minutes ago you said she is not on your mind!”(Lakini dakika zilizopita

ulisema hayupo akilini mwako)

“Let me just be brutally honest with you! I can’t stop thinking of Farida.”(Acha tu

niwe muaminifu kupita kiasi, siwezi kuacha kumfikiria Farida) niliongea

nikimwangalia Bianca, akainamisha kichwa chake chini kuonyesha maelezo yangu

yalimwumiza, lakini ilikuwa ni bora aumie akiwa ameambiwa ukweli.

Haikuwa rahisi kumsahau Farida, kila siku alisumbua akili na mawazo yangu,

mpaka wakati huo nilikuwa sijaamini kabisa kwamba alikuwa ni mfanyabiashara

wa dawa za kulevya, aliyekamatwa na madawa hayo nchini Saudia Arabia siku

chache tu kabla ya kumvisha pete ya uchumba na kilichokuwa kikisubiriwa ni

kupigwa risasi mbele za kadamnasi, hiyo ndiyo ilikuwa adhabu ya watu

waliokamatwa na madawa hayo katika nchi za Uarabuni.

“Lakini aliondoka kwa lengo la kwenda kufanya usaili ili ajiunge na Chuo Kikuu

cha Riyadh, naye akitamani awe angalau na digrii na familia yangu iweze

kumkubali. Alifanya kila kilichowezekana ili wazazi wangu wampende. Hivi ni

kweli Farida alikuwa akifanya biashara ya madawa?” nilijiuliza bila kupata majibu.

Ingawa Bianca alikuwa kando yangu, tena siku ya harusi yetu bado kichwani

mwangu alikuwemo Farida, fikra za kwamba angekuwa amekwishapigwa risasi

mpaka wakati huo zilinisumbua sana kiasi cha kunifanya nisifurahie kitu chochote

kilichokuwa kikiendelea ukumbini ingawa karibu kila mtu alishangilia mimi na

Bianca kufunga ndoa. Nilichotaka kufanya wakati huo ni kuondoka ukumbini

kwenda chumbani kupumzika.

Ghafla nilisikia mlio wa ujumbe wa simu kwenye simu yangu, nikijua ni kutoka

kwa baadhi ya rafiki zangu waliokuwa wakinitumia ujumbe wa pongezi.

Nilinyoosha mkono na kuichukua simu yangu mezani, kisha kufungua sehemu ya

ujumbe na kuanza kusoma, moyo wangu ulishtuka nilipoona maneno “Siri kubwa”.

Nikazidi kusogea chini ambako kulikuwa na anuani ya barua pepe ya Bianca, pia

ikiwa na alama yake ya siri ya kufungulia kama kuna mtu alitaka kusoma. Chini

yake kukiwa na maandishi “Tumekuletea hii, ili uingie kwenye sanduku la barua

pepe la mkeo, ili upate kumwelewa vizuri na unyama aliomfanyia Farida.”

Moyo wangu ukaruka mapigo kadhaa, jasho likaanza kunitoka, huku nikihisi kama

vile shinikizo langu la damu lilikuwa likishuka kwa kasi. Sikutaka tena kukaa

ukumbini, ujumbe huo wa simu ndio ulichochea kabisa hamu yangu ya kuondoka

kwenda chumbani kupumzika ambako lengo langu lilikuwa ni kwenda moja kwa

moja kwenye kompyuta na kufungua anuani ya barua pepe ya Bianca na kujionea

kilichokuwemo ndani. Moyoni nilijawa na hofu, nikiogopa ambacho ningekikuta

lakini bado nilitamani kujua.

“Sijisikii vizuri!” nilimgeukia Bianca na kumweleza.

“Nini tena?”

“Nataka kwenda kupumzika, ni vizuri tukaondoka.”

“Genesis, tuondoke mapema kiasi hiki? Kabla wazazi hawajaondoka?”

“Naumwa!” nilitoa kisingizio huku nikigeuza kichwa kuongea na Kelvin, mpambe

wangu wa siku hiyo. Mimi na Kelvin tulisoma pamoja Chuo Kikuu cha St. Augustine

kilichopo mjini Mwanza, alikuwa rafiki yangu mkubwa na tulishirikiana mambo

mengi.

“Vipi tena?” aliniuliza.

“Aisee mwambie MC atangaze kuwa tunaondoka kwenda chumbani kupumzika.”

“Eti shemeji?” Kelvin alimuuliza Bianca.

“Kama yeye ameamua mimi sina kizuizi”

Bila kipingamizi Kelvin alifanya kama alivyoombwa, MC akatangaza juu ya

kuondoka kwetu na watu wote wakasimama huku wakishangilia, tukitembea kwa

madaha tukiwa tumeshikana mikono kuelekea nje ya ukumbi ambako tuliingia

kwenye lifti na kwenda moja kwa moja ghorofa ya tatu, kilipokuwa chumba chetu,

Kelvin na mke wake Martina walikuwa pamoja na sisi mpaka ndani ambako bila

kuchelewa walituaga na kuondoka.

Kitu cha kwanza nilichofanya ni kwenda kwenye kompyuta yenye mtandao wa

Internet, haraka nikaiwasha na kuingia kwenye tovuti ya G-mail nikaandika

Bianca10@Gmail.com, kisha kwenye alama ya siri nikaandika neno Hadohado,

hiyo ndiyo ilikuwa alama ya siri ya Bianca. Niliyafanya yote hayo akiwa amejilaza

kitandani, bila kunisogelea. Nikabonyeza sehemu iliyoandikwa Sign in, muda

mfupi tu baadaye sanduku lake la barua pepe likafunguka, iliyokuwa juu kabisa

iliandikwa “The truth about innocent Farida Mbaraka”

Maneno yaliyomaanisha ukweli kuhusu Farida Mbaraka asiye na hatia. Moyo

wangu ukapiga kwa kasi, jasho likinitoka huku nikisubiri ifunguke, sekunde

chache baadaye kila kitu kilikuwa wazi nikaanza kusoma huku nikibubujikwa na

machozi, mara kadhaa niligeuza shingo yangu kumwangalia Bianca aliyekuwa

amejilaza kitandani, hasira ikazidi kunipanda zaidi na zaidi, nilimwonea Farida

huruma kiasi cha kutamani kuua, hakustahili unyama aliotendewa kwa sababu

yangu. Sikumchukia Bianca peke yake bali pia familia yangu.

Hatimaye nikafikia uamuzi wa kufanya nilichoona kinafaa, kama Farida alikuwa

ameshapigwa risasi sababu ya madawa ya kulevya ambayo hakuyamiliki, basi

waliofanya mpango huo nao hawakustahili kuishi hata kama walikuwa ni ndugu

zangu na wa kwanza kufa alitakiwa kuwa Bianca! Nikanyanyuka nilipokuwa

nimeketi na kutembea mpaka kwenye meza iliyokuwa pembeni, juu yake

kulikuwa na sinia lenye chakula, pia vikiwepo visu na uma.

“Hiki kinatosha!” niliwaza wakati nakichukua kisu na kuanza kutembea taratibu

kuelekea kitandani alipolala Bianca akiwa hajui kilichoendelea, nikahesabu moja

mpaka tatu kisha kushusha mkono kwa kasi kifuani kwake upande wa moyo,

damu nyingi ikaruka na kulowanisha nguo zangu, nikakichomoa tena na

kukizamisha mara ya pili kisha kuchukua mto na kumgandamiza nao Bianca

mdomoni ili kelele zake zisitoke nje, dakika tano baadaye alitulia, tayari

alishakufa.

“Mungu wangu nimefanya nini? Kwanini nimeua? Si ningemwacha tu na kutafuta

mwanamke mwingine?” niliwaza nikimwangalia, ilikuwa kama vile niliachiwa na

shetani aliyekuwa amenifunika na kuuona ukweli wa ubaya nilioutenda.

Lakini kwanini nimeua siku ya harusi yangu? Nimesoma nini kwenye barua pepe

hii?

Ilionekana kuwa siku ya furaha kubwa, Genesis mtoto wa tajiri alikuwa akimuoa

binti mrembo aitwaye Bianca, mtoto wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Watu

wote maarufu walikuwa ndani ya ukumbi kushuhudia tukio hilo la kihistoria bila

kufahamu kuwa lingeishia kwenye mauaji, Genesis akiwa amemuua kwa

kumchoma kisu Bianca wakiwa chumbani, kisha yeye mwenyewe kujirusha

kupitia dirishani ili aanguke chini na kufa. Kwanini aliamua kufanya mauaji hayo

ya kikatili? Je, alipojirusha dirishani alikufa?

Genesis anasimulia historia ya maisha yake, jinsi alivyozaliwa kwenye familia ya

wasomi ambao hata siku moja hawakukubaliana na suala la mtoto wao kuoa au

kuolewa na mtu asiyekuwa msomi. Akiwa kidato cha pili katika shule ya kimataifa

ya Mtakatifu Thomas mkoani Morogoro, msichana mrembo aitwaye Farida

anahamia katika shule hiyo kutoka shule ya Sekondari ya Kilakala.

Kihistoria msichana huyu anatoka familia maskini sana, wazazi wake hawakupata

elimu hata kidogo. Pamoja na hayo, Farida alikuwa na akili nyingi kupita kiasi,

zilizomfanya ashike namba moja kwenye mtihani wa taifa Tanzania nzima. Tukio

hili ndiyo lilimfanya Padri Bathromayo wa Shirika la Kitume la Women Oppotunity

Expanded, aamue kumhamisha Farida kutoka Kilakala kwenda shule ya Sekondari

ya Mtakatifu Thomas, gharama zote za masomo yake zikichukuliwa na shirika hilo.

Baada ya kutambulishwa darasani, Farida akatokea kuwa rafiki mkubwa wa

Genesis pamoja na kijana mwingine aitwaye Chris. Katika mazungumzo yao,

Farida ambaye ameitingisha shule hiyo kwa uzuri wake, wavulana wakiwa

wamepania kumpata, aligundua Genesis ni mtoto kutoka familia tofauti sana na

yake kiuchumi lakini hakuwa na majivuno na alikuwa muungwana.

Je, nini kitaendelea?

Simulizi : Kifo Siku Ya Harusi Yangu Sehemu Ya pili (2)

Umeipenda? Dondosha coment kama unataka tuendelee na episode inayofuata

Comments

Popular posts from this blog

AirPods Fake Vs Real – How To Spot Fake AirPods In 2021 (Ultimate Guide)

AirPods Fake Vs Real – How To Spot Fake AirPods In 2021 (Ultimate Guide) Need your item authenticated by us? Proven expertise, not self-claimed. Get checked by the industry's top experts. Get Authenticated Want this item? Buy it from our partners! Looking to learn how to spot fake AirPods? Scared of getting scammed? Look no further, as we’ve compiled the most complete legit check guide for Apple AirPods. To put it shortly, the quickest way to spot fake AirPods is to scan the serial number found on the inside of the case (see pictures below on how to find that serial number). Once you get that code, pop it through  checkcoverage.apple.com  and see whether Apple confirms it for you. If you can’t get ahold of this code, we’ve added fake vs real comparisons for the actual AirPods below! Remember, fake AirPods will always compromise on quality. To highlight the most common places where these compromises are made, we’ve put together the comparisons you’ll find below. In this guide we'

Breaking news: Haji S. Manara ahamia yanga

  Aliekua msemaji mkuu wa Simba SC maarufu H. S. Manara. Baada ya kutokea kutokuelewana na klabu yake aliyokua akiitumikia, leo tar 24 August 2021 ametambulishwa rasmi Yanga SC na ya kusaini kandarasi akiwa kama msemaji huru.  Nimekiwekea baadhi ya matukio bofya kuangalia. Tujikumbushe pia enzi akiwa Simba SC. 

Aina ya sita ya vyakula ambavyo vikichanganywa hugeuka sumu

  Aina ya sita ya vyakula ambavyo vikichanganywa hugeuka sumu Kila binadamu ana kile alichojaaliwa na Mungu. Siku zote anachoamua mmoja kula huenda kikawa sumu kwa mwingine. Chakula anachokula mtu kinaenda sanjari na hali ya kiafya. Wengine huumwa hadi kusababisha kupoteza uhai na hii ni baada tu ya kupendelea kuchanganya chakula. Mtu mmoja anaweza kula sawa na kwa urahisi, ila kwa mwingine kikageuka sumu. Hali hii huchochewa zaidi na matokeo ya baadae pale unaposhindwa kuweka mchanganyiko sahihi na wenye afya zaidi . Kila aina chakula ina faida zake, ila kinapochanganywa kinaweza kusababisha shida kwa mtu. Kwa watu ambao wanataka kuchanganya lishe ili kupunguza unene na vichocheo vyake ni vyema kushauriana na wataalamu jinsi ya kupanga lishe bora. Mtaalam wa lishe wa Nigeria Habiba Haruna ameiambia BBC kuhusu aina sita za chakula ambazo zinaweza kuwa sumu kwa mtu yeyote. Samaki na Maziwa Samaki na Maziwa ni vyakula vyenye virutubisho lukuki na kuvichanganya katika sehemu moja vinaweza