Skip to main content

Posts

Showing posts with the label simulizi

Simulizi : Kifo Siku Ya Harusi Yangu Sehemu Ya Pili (2)

  Ilipoishia  Simulizi : Kifo Siku Ya Harusi Yangu Sehemu Ya Kwanza (1) Baada ya kutambulishwa darasani, Farida akatokea kuwa rafiki mkubwa wa Genesis pamoja na kijana mwingine aitwaye Chris. Katika mazungumzo yao, Farida ambaye ameitingisha shule hiyo kwa uzuri wake, wavulana wakiwa wamepania kumpata, aligundua Genesis ni mtoto kutoka familia tofauti sana na yake kiuchumi lakini hakuwa na majivuno na alikuwa muungwana.    Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO.    Huo ndio ulikuwa mwanzo, sumaku ya mapenzi ilionekana kuwavuta karibu kadri siku zilivyozidi kusonga ingawa wote wawili walipambana nayo. Mpaka umri huo wote walikuwa bikira, kama hivi ndivyo hata wanaume wanaweza kuitwa kama hawajakutana na mwanamke kimwili! Genesis tangu kuzaliwa kwake alikuwa bado hajamjua mwanamke, kwani aliamini kufanya hivyo ilikuwa ni dhambi kubwa ambayo mtu alistahili kuchomwa moto siku ya mwisho, hivyo ndivyo alivyofundishwa na wazazi wake na pia kanisani siku za Jumapili.    Ilikuwa hivyo pia k

Simulizi : Kifo Siku Ya Harusi Yangu Sehemu Ya Kwanza (1)

Simulizi : Kifo Siku Ya Harusi Yangu Sehemu Ya Kwanza (1) IMEANDIKWA NA : ERIC SHIGONGO ******************************************************************************** Simulizi : Kifo Siku Ya Harusi Yangu Sehemu Ya Kwanza (1) MWANZO Mamia ya watu walikuwa wamefurika ndani ya ukumbi wa Pundamilia ulio ndani ya hoteli ya maarufu ya Atrium, karibu kila mtu maarufu nchini Tanzania alikuwa ndani ya ukumbi huu. Kuanzia Rais, Mawaziri, Makatibu Wakuu, wanamichezo, wasanii na wafanyabiashara wakubwa wa Kiasia na Afrika. Hakika ilionekana siku ya furaha, watu wakiwa wameketi kwenye meza zao wakiendelea kunywa vinywaji taratibu. Wanaume wakiwa wamevalia suti nyeusi na wanawake magauni ya rangi nyeupe na zambarau, hakika walipendeza. Kila nilipozungusha macho yangu huku na kule ndani ya ukumbi nilionekana kutoamini kilichokuwa kinatendeka, hatimaye  baada ya safari ndefu ya kupanda na kushuka milima, nilikuwa namuoa Bianca Rwegoshora, mtoto wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Ja